Wazriri wa Fedha na mipango Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa sababu za ongezeko la kodi kwenye miamala ya simu kwa mitandao yote.
Amesema hayo alipokuwa katika mahojiano na idhaa ya Taifa TBC1,na kuongeza kuwa kufanya hivyo ni kutokana na kuwepo kwa changamoto nyingi za upungufu wa Miundombinu kwenye sekta mbali mbali ( Hospitali,Shule,Barabara, Vivuko, nk.)
Aidha Dkt Nchemba amesema kuwa kumekuwepo na shida kwenye mahospitali hususani vitanda, wodi, nk,hali inayopelekea adha kubwa kwa mama wajawazito kupoteza maisha au vichanga.
FULL STORY TUMEKUWEKEA VIDEO YAKE HAPA
https://www.youtube.com/watch?v=Xt67xpzaBS0

0 Comments